Ibenge atabiri mechi ngumu dhidi ya Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th November 2024


Ibenge atabiri mechi ngumu dhidi ya Yanga

Kocha Mkuu wa Al Hilal Florent Ibenge amesema mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Yanga ambao utapigwa kesho Jumanne katika uwanja wa Benjamin Mkapa, utakuwa mgumu kwa kila upande

Ibenge amesema katika kundi A kila timu ina nafasi ya kusonga mbele hivyo anatarajia kila mechi watakayocheza iwe nyumbani au ugenini itakuwa ngumu

Aidha Ibenge amebainisha kuwa awali walijiandaa dhidi ya Yanga iliyokuwa ikinolewa na Kocha Miguel Gamondi lakini sasa wanakwenda kucheza dhidi ya Yanga inayonolewa na kocha mpya. Mabadiliko hayo ya benchi la ufundi yaliyofanywa na Yanga, yameongeza ugumu wa mchezo huo

"Sisi tuko tayari kwa mchezo huu ambao tunatambua hautakuwa mwepesi. Katika kundi letu kila timu ina nafasi ya kusonga mbele hivyo tumejiandaa kukabiliana na upinzani tutakaokutana nao katika kila mchezo"

"Tumekuja tumejiandaa na tumeitazama Yanga na kuichambua kwa kina lakini ghafla wakabadili kocha. Nina imani mechi itakuwa ngumu sababu bado hatujajua na hatujaona mbinu za kocha mpya wa Yanga ila tumejiandaa kwa asilimia kubwa wachezaji wangu wako tayari kupambana hapo kesho"

"Yanga wana wachezaji wazuri timu Ikiwa na Maxi, Pacome, na Azizi ki NI ngumu kuzuia wasipate bao ila tumekuja kusaka alama tatu hatujaja kwaajili ya kupoteza mechi maandalizi yetu tumefanya kwaajili ya ushindi," alisema Ibenge

Yanga, Al Hilal, TP Mazembe na MC Alger ziko kundi A katika michuano ya ligi ya mabingwa hatua ya makundi ikianza kutimua vumbi kesho

Wakati Yanga ikichuana na Al Hilal, kule DR Congo TP Mazembe watakuwa wakiumana na MC Alger


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.