Klabu ya Singida Black Stars jana ilitangaza kuwasimamisha makocha wake wawili, Patrick Aussems na msaidizi wake Dennis Kitambi kutokana na matokeo mabaya, huku ikidaiwa kumwania Miguel Gamondi aliyeachana na Yanga hivi karibuni
Baada ya matokeo ya sare ya mabao 2-2 na Tabora United kwenye Uwanja wa Al Hassan Mwinyi, mchezo wa Ligi Kuu Bara, Singida BS ilitangaza kuwasimamisha makocha hao kutokana na matokeo mabaya ya timu hiyo, ambayo imepoteza mchezo mmoja na kutoka sare miwili kati mechi 11 iliyocheza chini ya makocha hao
Wakati Aussems na msaidizi wake wakiwekwa kando kuna taarifa kuwa Gamondi amekuwa akitajwa kuwa anaweza kwenda kurithi mikoba ya Mfaransa huyo aliyeiongoza Singida katika michezo 10 ya Ligi Kuu Bara akiwa ameshinda saba, ametoka sare miwili na kupoteza mmoja tu dhidi ya Yanga
Timu hiyo ipo nafasi ya nne ikiwa na pointi 24 sawa na Yanga na Azam, ikiwa imefunga mabao 15 na kuruhusu sita
Gamondi aliondolewa Yanga Novemba 15, 2024, baada ya uongozi wa timu hiyo kusema kuwa hairidhishwa na matokeo ya timu hiyo ambayo ilikuwa haijapata ushindi kwenye mechi mbili mfululizo akiwa aliipa ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita



