Yanga imeanza vibaya hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa barani Afrika ikikubali kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya Al Hilal katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Mabao ya kipindi cha pili yaliyofungwa na Adama Colibaly na Yassir Mozamir yametosha kumuhakikishia kocha Florent Ibenga ushindi muhimu ambao umeipeleka Al Hilal kileleni mwa kundi A
Kocha wa Saed Ramovic ana kazi ya kufanya kwani kikosi chake hakikutengeneza nafasi nyingi licha ya Kennedy Musonda kukosa nafasi adimu katika kipindi cha pili mpira wake wa kichwa ukigonga mwamba
Katika mchezo mwingine wa kundi A uliopigwa DR Congo, TP Mazembe imelazimishwa suluhu ya bila kufungana dhidi ya MC Alger
Al Hilal wanaongoza kundi A wakiwa na alama tatu huku Mazembe na MC Alger zikifuatia na alama moja na Yanga kuburuza mkia
Ni mchezo wa tatu mfululizo Yanga inapoteza katika mashindano yote



