Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mchezo mmoja unatarajiwa kupigwa uwanja wa Azam Complex Azam Fc wakiwa wenyeji wa Singida Black Stars
Ni mechi ya kuamua nani anakaa nafasi ya pili kati ya timu hizo ambazo zote zimekusanya alama 24 baada ya kuchez mechi 11
Azam Fc wana uwiano mzuri wa mabao, wanaishikilia nafasi hiyo kwa sasa mbele ya Yanga na Singida BS
Ushindi kwa Azam Fc utawafanya wasogee karibu zaidi ya Simba inayoongoza ligi ikiws na alama 28 lakini hata matokeo ya sare yatawabakisha katika nafasi hiyohiyo
Lakini kama Singida BS watashinda watasogea hadi nafasi ya pili, sare itawasogeza nafasi ya tatu lakini wakipoteza watasailia katika nafasi yao
Singida BS wako chini ya Kaimu Kocha Mkuu Ramadhan Nsanzurwimo aliyechukua mikoba ya Patrick Aussems aliyetimuliwa baada ya kukosa ushindi katika mechi tatu mfululizo
Mtangane huo unatarajiwa kupigwa saa 1 usiku..




