Local,Normal News,Fountain

Fountain Gate yawasimamisha Barthez, Abalkassim

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Nov 2024
Fountain Gate yawasimamisha Barthez, Abalkassim

Kocha wa makipa wa Fountaine Gate, Ally Mustapha 'Barthez' na kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Abalkassim Suleiman wamekiri kusimamishwa na klabu hiyo kwa sababu mbalimbali huku Desemba 6 mwaka huu uongozi ukitarajia kukaa kikao cha kuwajadili

Barthez na Abalkassim walisimamishwa siku moja baada ya timu hiyo kufungwa na Pamba Jiji mabao 3-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa Novemba 5 mwaka huu kwenye Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Manyara

Mchezaji Abalkassim amethibitisha kupokea barua yenye makosa mawili"

"Ni kweli nipo nje ya timu na nilipokea barua ya kusimamishwa kwa kosa la kuondoka kambini bila ruhusa lakini pia natuhumiwa kuwa nilicheza vibaya kwenye mchezo dhidi ya Pamba ambao nilionyeshwa kadi nyekundu wakidai kuwa nilifanya makusudi," alisema kiungo huyo na kuongeza

"Baada ya wiki mbili kupita niliwapigia viongozi juu ya sakata hilo niliomba kuonana nao ili wanipe barua ya kuachana na timu kutokana na hayo madai, sikupewa na zaidi wamenitaka nikutane nao tena Desemba 6 mwaka huu kwaajili ya kikao cha kunijadili."

Kwa upande wa Bartez alisema hafahamu sababu za kusimamishwa kwake bali anachoweza kusema yupo nje ya timu hiyo kwa muda anaendelea na shughuli nyingine

"Nafikiri watu sahihi wa kuzungumza nao juu ya sababu za mimi kuondoka ndani ya timu ni viongozi, mimi nipo Dar es Salaam kwa sababu nimeondolewa kwenye majukumu yangu sifahamu sababu ni nini," alisema Barthez ambaye aliwahi kuwa kipa wa Simba na Yanga kabla ya kugeukia katika ukocha.

Mwanaspoti

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
59m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’