Azam Fc imezidi kuisogelea Simba kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya leo kuichapa Singida Black Stars mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex
Alikuwa ni Feisal Salum 'Fei Toto' aliyeitanguliza Azam Fc mapema kipindi cha kwanza akifunga bao lake la tatu msimu huu baada ya kuunganisha krosi ya Iddi Nado
Azam Fc ilitawala mchezo katika kipindi cha kwanza na ilienda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0
Singida BS walizinduka katika kipindi cha pili lakini ni Azam Fc waliokuwa hatari zaidi kupitia mashambulizi yao ya kushitukiza
Jhonier Blanco akawaongezea bao la pili katika dakika ya 57 akimalizia shambulizi la kushitukiza
Bao pekee la kufutia machozi upande wa Singida BS lilifungwa na Elvis Rupia aliyefunga bao lake la tano msimu huu
Ushindi huo umeifanya Azam Fc ifikishe alama 27 katika nafasi ya pili ikiwa nyuma ya vinara Simba kwa tofauti ya alama 1
Singida BS wamesalia katika nafasi ya nne, walima alizeti hao wakicheza mechi ya nne pasipo kupata ushindi



