Local,Normal News,Azam, Singida

Azam Fc yaichapa Singida BS 2-1

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Nov 2024
Azam Fc yaichapa Singida BS 2-1

Azam Fc imezidi kuisogelea Simba kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya leo kuichapa Singida Black Stars mabao 2-1 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex

Alikuwa ni Feisal Salum 'Fei Toto' aliyeitanguliza Azam Fc mapema kipindi cha kwanza akifunga bao lake la tatu msimu huu baada ya kuunganisha krosi ya Iddi Nado

Azam Fc ilitawala mchezo katika kipindi cha kwanza na ilienda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0

Singida BS walizinduka katika kipindi cha pili lakini ni Azam Fc waliokuwa hatari zaidi kupitia mashambulizi yao ya kushitukiza

Jhonier Blanco akawaongezea bao la pili katika dakika ya 57 akimalizia shambulizi la kushitukiza

Bao pekee la kufutia machozi upande wa Singida BS lilifungwa na Elvis Rupia aliyefunga bao lake la tano msimu huu

Ushindi huo umeifanya Azam Fc ifikishe alama 27 katika nafasi ya pili ikiwa nyuma ya vinara Simba kwa tofauti ya alama 1

Singida BS wamesalia katika nafasi ya nne, walima alizeti hao wakicheza mechi ya nne pasipo kupata ushindi

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’