Local,Normal News,Azam

Azam Fc mechi 6, alama 18

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 Nov 2024
Azam Fc mechi 6, alama 18

Ushindi wa Azam FC wa mabao 2-1 ilioupata juzi dhidi ya Singida Black Stars kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara imeifanya kuondoka na pointi tatu katika michezo sita mfululizo, huku Kocha Mkuu wa timu hiyo, Rachid Taoussi akisema kwa sasa timu yake ni imara

Tangu ilipolazimishwa suluhu dhidi ya Mashujaa FC kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Septemba 29 mwaka huu, Azam ikaanza kupata ushindi mfululizo hadi kufikia michezo sita kwa kuifunga Namungo bao 1-0, ikaishindilia Prisons mabao 2-0, ikaipa kipigo cha mabao 4-1, KenGold, kabla ya kuichapa Yanga bao 1-0, baada ya hapo ikaifunga Kagera Sugar bao 1-0, kabla ya juzi kushinda mabao 2-1, mechi ikichezwa, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam

Katika michezo hiyo, dhidi ya Namungo, Prisons na Yanga ilicheza ugenini, huku dhidi ya KenGold, Kagera Sugar na Singida Black Stars ikiwa nyumbani

Azam imecheza michezo saba bila kupoteza, ambapo mara ya mwisho ilifungwa mabao 2-0 dhidi ya Simba, Septemba 26 kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar, baada ya hapo ikatoka suluhu dhidi ya Mashujaa FC na kuanza kushinda mfululizo

Kocha Mkuu wa Azam, Taoussi, amesema timu yake kwa sasa imeimarika kwa kutosha, lakini pia amewatahadharisha wachezaji wake kuendelea kuwa makini

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’