Local,Normal News,Simba

Malengo ya Simba ni ushindi tu - Ahmed

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 Nov 2024
Malengo ya Simba ni ushindi tu - Ahmed

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amesema katika msimu huu Simba inacheza kwa malengo zaidi ya kusaka alama tatu kila mchezo ili kufanikisha mipango mikubwa waliyonayo

Licha ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Bravos ya Angola katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi kombe la Shirikisho (CAF CC), kumekuwa na ukosoaji juu ya kiwango kilichoonyeshwa na Simba katika mchezo huo

Ahmed amesema michuano hiyo inahitaji zaidi matokeo ya ushindi kuliko maonesho

"Sisi Tumefurahia ushindi tulioupata kwa kuiheshimisha nchi, hii ni michuano ya Afrika, tunachohitaji ni kukusanya pointi tatu kwa maana hiyo tumetimiza malengo"

"Mashindano haya hayahitaji mbwembwe. Kuna wengine wanatubeza kuwa tumepata bao la penalti, lakini wakumbuke kuwa hata kufunga kwa penalti nako kunahitaji umahiri na ufundi"

"Ndiyo maana Simba ilipata penalti yake Ahoua akafunga, wenzetu wakapata lakini kipa wetu Moussa Camara akaokoa, hii yote ni kuonesha tuna wachezaji wenye uwezo, ubora na vipaji, siyo kila penalti ikipatikana basi unaweza kufunga," alisema Ahmed

Ushindi huo uliihakikishia Simba kukusanya alama tatu za kwanza kwenye michuano ya CAF CC msimuu ikiongoza kundi A sambamba na CS Constantine ya Algeria

Mchezo unaofuata Disemba 08 Simba itakuwa ugenini Algria kumenyana na CS Constantine

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
4h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
11h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
14h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
14h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
16h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’