Kikosi cha Yanga kinatarajiwa kuondoka nchini leo kuelekea Algeria kwa ajili ya mchezo wa raundi ya pili hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika (CAF CL)
Jumamosi, Disemba 07 Yanga itamenyana na MC Alger katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Julai 05 huko Algeria
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema timu itaondoka leo Jumanne, jioni
Yanga ilipoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Al Hilal hivyo mabingwa hao wa Tanzania Bara wanakwenda Algeria kusaka ushindi ili kuweka hai matumaini ya kufuzu robo fainali
Wako nafasi ya nne katika kundi A linaloongozwa na Al Hilal yenye alama tatu huku MC Alger na TP Mazembe zikifuatia na alama moja baada ya mchezo baina yao kumalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana wiki iliyopita



