Yanga kuifuata MC Alger leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd December 2024


Yanga kuifuata MC Alger leo

Kikosi cha Yanga kinatarajiwa kuondoka nchini leo kuelekea Algeria kwa ajili ya mchezo wa raundi ya pili hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika (CAF CL)

Jumamosi, Disemba 07 Yanga itamenyana na MC Alger katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Julai 05 huko Algeria

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema timu itaondoka leo Jumanne, jioni

Yanga ilipoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Al Hilal hivyo mabingwa hao wa Tanzania Bara wanakwenda Algeria kusaka ushindi ili kuweka hai matumaini ya kufuzu robo fainali

Wako nafasi ya nne katika kundi A linaloongozwa na Al Hilal yenye alama tatu huku MC Alger na TP Mazembe zikifuatia na alama moja baada ya mchezo baina yao kumalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana wiki iliyopita


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.