Jude Bellingham na Kylian Mbappe juzi walifunga mabao ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Getafe na kuifanya Real Madrid wakizidi kusogea kileleni mwa msimamo wa ligi sasa wakitofautiana alama moja tu na kinara wa LaLiga Barcelona wakiwa na mchezo mkononi
Baada ya Barca kuchapwa mabao 2-1 na Las Palmas, Los Blancos walifunga bao la kwanza kupitia mkwaju wa penalti, Bellingham hakufanya makosa baada ya Allan Nyom kuadhibiwa kwa kumchezea vibaya Antonio Rudiger
Bellingham kisha akageuka mtoa huduma huku Madrid wakiongeza bao la pili dakika nane baadaye kwa kumpata nahodha wa Ufaransa, ambaye alipiga mpira nje ya eneo la hatari kwa bao lake la 10 msimu huu, akifunga katika mechi mfululizo za ligi kuu kwa mara ya kwanza tangu Septemba
Madrid sasa imeshinda kila mechi kati ya 16 zilizopita za LaLiga dhidi ya Getafe
Real Madrid sasa wanahitaji kushinda mechi yao ya kiporo ili kurejea kileleni mwa msimamo wa ligi na kuindoa Barca ambayo karibuni imekosa ushindi katika mechi tatu mfululizo za La Liga