Young uso kwa uso na mwanae kombe la FA

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd December 2024


Young uso kwa uso na mwanae kombe la FA

Mchezaji wa Everton, mkongwe Ashley Young atakabiliana na mtoto wake wa miaka 18, Tyler kwenye michuano ya Kombe la FA

Everton imepangwa kumenyana na Peterborough United kwenye Raundi ya Tatu ya Kombe la FA, uwanjani Goodison Park, Januari 11 mwakani

Hiyo inamaana staa huyo wa zamani wa Manchester United, Ashley, 39, atakwaana jino kwa jino na mtoto wake, ambaye anacheza kwenye League One akicheza kikosi cha Under-21 cha Petersborough

Na Young amefurahia jambo hilo kupata nafasi ya kucheza dhidi ya mwanaye akiandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii kuwa ndoto imetimia


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.