Local,Normal News,Singida

Aussems awashukia viongozi Singida BS

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 Dec 2024
Aussems awashukia viongozi Singida BS

Aliyekuwa kocha wa Singida Black Stars Patrick Aussems amewaaga wanafamilia wa timu hiyo baada ya mkataba wake pamoja na kocha msaidizi kusitishwa ghafla wiki iliyopita

Katika salamu zake za shukrani, Aussems amewashushia lawama viongozi wa Singida BS kuwa wamekosa weledi wa kuiendesha tmu hiyo

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa  kijamii, Aussems ameandika ujumbe huu;

"Hakika maamuzi yaliyofanyika hayakua kwa sababu ya matokeo. Ilikua furaha kufundisha kundi hili la wachezaji. Lakini Ilikua ni kama jinamizi kila siku kufanya kazi na uongozi usiokua na weledi"

"Nilikua nikilalamikia kila siku kuhusu kukosekana kwa uwezo katika uongozi. Msaidizi wangu, Denis Kitambi na mimi binafsi hatujashangazwa na maamuzi yaliyofikiwa, ilikua ni kama ahueni kwetu"

"Hivyo nadhani sasa mmeshaelewa tatizo lilikua wapi. Ningependa kuwashukuru maelfu ya watu kila kona ya nchi kwa miezi mitano iliyopita waliokuja kwangu kunitakia heri, na kupiga na mimi selfie"

"Najiona bado nilikua napendwa sana na mashabiki wa Simba pamoja na watu wengine pia. Nathamini sana wema na ukarimu wenu. Mwisho, kama isemavyo methali ya kifaransa 'Jamais 2, Sans 3'. Kwa maana ya kuwa jambo ambalo limeshatokea mara mbili nyuma upo uwezekano litatokea mara ya tatu siku za mbeleni. Hivyo labda inawezekana tutaonana tena hivi karibuni," aliandika Aussems

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
11h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
17h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
23h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’