Local,Normal News,Simba

Simba yapaa Algeria na matumaini kibao

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Dec 2024
Simba yapaa Algeria na matumaini kibao

Kikosi cha Simba kimeondoka nchini alfajiri ya leo Jumatano kuelekea Algeria kwa ajili ya mchezo wa raundi ya pili hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho la CAF dhidi ya CS Constantine

Mchezo huo utapigwa Jumapili, Disemba 08, saa 1 usiku

Akizungumza muda mfupi kabla ya kuanza safari, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali alitamba kuwa wanakenda Algeria wakiwa na dhamira moja tu, kusaka alama tatu katika mchezo huo

Ahmed amewataka wapenzi, wanachama na mashabiki wa timu hiyo kuwaombea ili waweze kufika salama na hatimaye kutetea vyema bendera ya Tanzania katika mchezo huo

Simba itasafiri kwa takribani siku mbili kwani imetoka Dar es salaam na kutarajiwa kutua Instabul, Uturuki leo ambapo kesho Alhamisi wataunganisha ndege nyingine kuelekea Algiers

Wakifika Algiers, Simba wataanza safari nyingine kuelekea mji wa Constantine ambapo ni mwendo wa takribani saa 5 kwa basi na saa 1 na dakika 40 kwa ndege

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
3h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
7h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
13h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
13h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
13h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
15h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
19h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’