Mlinda lango wa Simba Aishi Manula alikuwa miongoni mwa wachezaji waliokuwa wakisafiri kuelekea Algeria kwa ajili ya mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya CS Constantine ambao utapigwa Jumapili, Disemba 08
Hata hivyo Manula alipata changamoto ya kiafya muda mfupi kabla ya kuanza safari na hivyo kushindwa kusafiri
Klabu ya Simba imethibitisha kwa mlinda lango huyo kushindwa kuungana na wenzake katika safari
Simba imewasili Instabul na inatarajiwa kuunganisha ndege nyingine kuelekea Algeria



