Simba yataja sababu ya Manula kutosafiri Algeria

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th December 2024


Simba yataja sababu ya Manula kutosafiri Algeria

Mlinda lango wa Simba Aishi Manula alikuwa miongoni mwa wachezaji waliokuwa wakisafiri kuelekea Algeria kwa ajili ya mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya CS Constantine ambao utapigwa Jumapili, Disemba 08

Hata hivyo Manula alipata changamoto ya kiafya muda mfupi kabla ya kuanza safari na hivyo kushindwa kusafiri

Klabu ya Simba imethibitisha kwa mlinda lango huyo kushindwa kuungana na wenzake katika safari

Simba imewasili Instabul na inatarajiwa kuunganisha ndege nyingine kuelekea Algeria


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.