International,Normal News,Leicester, Manchester United

Nistelrooy hakufurahia kutemwa Man United

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Dec 2024
Nistelrooy hakufurahia kutemwa Man United

Kocha mpya wa Leicester Ruud van Nistelrooy amesema hakutaka kuondoka Manchester United akiwa na alitamani kubakia, lakini kwa sasa anaweka nguvu katika klabu yake mpya

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Mashetani Wekundu alichukua nafasi ya Steve Cooper siku ya Ijumaa, na kusaini mkataba hadi 2027

Hatua hii inakuja baada ya kocha huyo kuiongoza Man United katika michezo minne kama meneja wa muda Old Trafford, kufuatia kufukuzwa kwa Erik ten Hag

Van Nistelrooy, aliyeletwa na Ten Hag kama meneja msaidizi mwezi Julai, alisimamia ushindi mara tatu na sare moja na kuna maneno kuwa alikasirishwa na kuondoka kwake

"Wakati nilipochukua kazi ya muda nilisema niko hapa kusaidia United na ningependa kubaki kuisaidia United, na nilimaanisha hivyo. Kwa hivyo nilisikitishwa sana, na iliniuma ilinibidi kuondoka, nilitamani kubaki kuleta mabadiliko katika klabu yangu ya zamani"

"Lakini nafarijika kuona United ipo chini ya kocha salama kwa sababu pia ninamuelewa meneja mpya. Nilizungumza na Ruben kuhusu hilo, sawa kwake, mazungumzo yalikuwa ya kushukuru, kati ya meneja," alisema

Van Nistelrooy aliiongoza Leicester Jumanne usiku kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya West Ham United ukiwa ushindi wake wa kwanza siku mbili tangu alipojiunga na timu hiyo

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
3h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
3h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
4h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
5h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
5h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
6h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
6h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
20h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
21h ago
READ MORE β†’