Chikola mchezaji bora ligi kuu Novemba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th December 2024


Chikola mchezaji bora ligi kuu Novemba

Kiungo wa Ushambuliaji wa Klabu ya Tabora United Offen Chikola amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Mwezi Novemba wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara

Hii ni baada ya Kuwashinda Golikipa wa klabu ya Simba Moussa Camarra na Mshambuliaji wa klab ya Tabora United Yacouba Songne

Katika Michezo 4 ya mwezi Novemba waliyocheza Tabora United, Offen Chikola amekuwa Katika kiwango Bora Huku akifanikiwa kufunga Mabao Matatu (3) Katika Dakika 351 alizoshuka dimbani

Hii inakuwa Tuzo ya kwanza kwa Chikola tangu aanze kucheza ligi kuu ya NBC Tanzania Bara Katika Vilabu tofauti tofauti kama Geita Gold na Mtibwa Sugar

Kocha Mkuu Rachid Taoussi wa Azam FC amechaguliwa kuwa Kocha Bora wa mwezi Novemba pia, Kocha Rachid amewashinda makocha wenzake Fadlu Davies wa Simba na Hamad Ally wa JKT Tanzania


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.