Kiungo wa Ushambuliaji wa Klabu ya Tabora United Offen Chikola amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Mwezi Novemba wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara
Hii ni baada ya Kuwashinda Golikipa wa klabu ya Simba Moussa Camarra na Mshambuliaji wa klab ya Tabora United Yacouba Songne
Katika Michezo 4 ya mwezi Novemba waliyocheza Tabora United, Offen Chikola amekuwa Katika kiwango Bora Huku akifanikiwa kufunga Mabao Matatu (3) Katika Dakika 351 alizoshuka dimbani
Hii inakuwa Tuzo ya kwanza kwa Chikola tangu aanze kucheza ligi kuu ya NBC Tanzania Bara Katika Vilabu tofauti tofauti kama Geita Gold na Mtibwa Sugar
Kocha Mkuu Rachid Taoussi wa Azam FC amechaguliwa kuwa Kocha Bora wa mwezi Novemba pia, Kocha Rachid amewashinda makocha wenzake Fadlu Davies wa Simba na Hamad Ally wa JKT Tanzania




