Local,Normal News,Simba

Fadlu awafichia mbinu CS Constantine

Joel JJ By Joel JJ
5 Dec 2024
Fadlu awafichia mbinu CS Constantine

Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids amesema hatafanya mazoezi yoyote ya mbinu wakiwa Algeria ili kutowapa nafasi wapinzani wao, CS Constantine kufahamu mfumo watakoutumia 

Jumapili, Disemba 08 Simba itawavaa wenyeji CS Constantine katika mechi ya Kundi A ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAF CC)

Muda mfupi kabla ya Simba kuondoka Tanzania jana, Fadlu aliweka bayana kuwa aina ya mazoezi watakayofanya Algeria ni kuwaweka fiti kimwili wachezaji wake kwa kuchezea mpira tu

Fadlu alisema maandalizi yote muhimu ya mchezo huo yalimalizikia wakiwa Tanzania, kinachofanyika ugenini ni kuondoa uchovu wa safari

"Tutakachokifanya ni kuhakikisha wanakuwa sawa upande wa utimamu wa mwili tu, kwa sababu ni hatari kufanya mazoezi ya mbinu ya mchezo huo kwa sasa"

"Tulimaliza mazoezi ya kimbinu pamoja na kuyafanyia kazi mapungufu na ubora wa wapinzani wetu tukiwa Tanzania. Huku yatakuwa ni mazoezi ya kawaida tu ya kuweka miili sawa kwa sababu macho yatakuwa mengi kututazama, siwezi kufanya mazoezi ya kimbinu au chochote kile kinatachowafanya wapinzani wetu hata kuhisi tunacheza vipi," alisema 

Fadlu amesema anatarajia itakuwa mechi ngumu hivyo amewaandaa wachezaji wake vyema hasa eneo la kujilinda na hatari za wapinzani wao katika mechi hiyo ya kwanza ugenini

"Tunatakiwa tuwe vizuri zaidi katika eneo la kuzuia huku tukijiepusha kufanya makosa mengi. Tumefanya mazoezi ya kuimarisha safu ya ulinzi na nafasi ya kiungo wa kukaba kwa sababu tunacheza ugenini, pia tunatakiwa kushambulia kwa haraka tukiwa na mpira na kurudi mapema," aliongeza Fadlu

Simba na CS Constantine zilishinda mechi zao ya raundi ya kwanza kwa ushindi wa bao 1-0 hivyo mchezo huo unaweza kuamua timu itakayokaa kileleni

Matokeo ya ushindi yatakuwa matokeo bora zaidi kwa Simba ugenini lakini hata matokeo ya sare yataiweka Simba katika nafasi nzuri ya kukamilisha malengo yake ya kuzufu robo fainali

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
3h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
12h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
13h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
15h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →