Yondani kuongeza nguvu Pamba Jiji

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th December 2024


Yondani kuongeza nguvu Pamba Jiji

Klabu ya Pamba Jiji imekamilisha usajili wa beki mkongwe Kelvin Yondani 'Cotton', imefahamika

Yondani ametua Pamba Jiji akiwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba na Geita Gold iliyoshuka daraja msimu uliopita

Yondani hakuwa na timu tangu msimu uliopita kumalizika na sasa anakwenda kuungana na kocha wake wa zamani Fred Felix Minziro waliyefanya nae kazi kwa mafanikio kunako klabu ya Geita Gold misimu miwili nyuma

Yondani ataanza kuitumikia Pamba Jiji baada ya dirisha dogo la usajili kufunguliwa Disemba 16


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.