Makundi kombe la Dunia la klabu 2025

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th December 2024


Makundi kombe la Dunia la klabu 2025

Droo ya Klabu Bingwa Dunia imechezeshwa jana ambapo Mabingwa watetezi Manchester City watakutana na Juventus katika hatua ya makundi huku Chelsea wakikutana na timu ya Flamengo kutoka Brazil

Man City ambao waiifunga Fluminense kutoka Brazil kwenye fainali za msimu uliopita ilitwaa taji hilo kwa mara ya kwanza 2023, wataanza kutetea taji lao dhidi ya Wydad ya Morocco na pia kucheza na Al Ain kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu katika Kundi G

Huu hapa mpangilio wa makundi;

  • Kundi A: Palmeiras, FC Porto, Al Ahly, Inter Miami
  • Kundi B: Paris St-Germain, Atletico Madrid, Botafogo, Seattle Sounders
  • Kundi C: Bayern Munich, Auckland City, Boca Juniors, Benfica
  • Kundi D: Flamengo, Esperance Sportive de Tunisie, Chelsea, Club Leon
  • Kundi E: River Plate, Urawa Red Diamonds, Monterrey, Inter Milan
  • Kundi F: Fluminense, Borussia Dortmund, Ulsan, Mamelodi Sundowns
  • Kundi G: Manchester City, Wydad, Al Ain, Juventus Kundi
  • Kundi H: Real Madrid, Al Hilal, Pachuca, Salzburg.

  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.