Local,Normal News,Yanga

Ramovic anataka ushindi Algeria

Joel JJ By Joel JJ
β€’
6 Dec 2024
Ramovic anataka ushindi Algeria

Kocha Mkuu wa Yanga Sead Ramovic amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya MC Alger ambao utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja wa July 05 1962

Akizungumza katika mkutano na wanahabari, Ramovic amesema anatambua mchezo huo utakuwa mgumu kwani wanakwenda kucheza dhidi ya timu ngumu lakini anaamini katika ubora wa timu yake na ana imani watafanya vizuri katika mchezo huo

Ramovic amesema Yanga ina historia katika uwanja wa July 05, hivyo kesho itakuwa siku nyingine kwao kusaka ushindi

"Tunakwenda kucheza na timu ngumu, ina wachezaji bora na kocha mzoefu lakini upande wetu tuna kikosi chenye wachezaji bora sana, naamini itakuwa mechi nzuri yenye kuvutia"

"Yanga wana historia kwenye uwanja tutakaotumia kesho, walipoteza mchezo wa Fainali hapa kwa kanuni lakini naamini walishinda mioyo ya wapenda mpira hapa Algeria, kesho ni siku nyingine na tutakuja na nguvu nyingine ya kutaka kushinda mchezo," alisema Ramovic

Kocha huyo raia wa Ujerumani ameongeza kuwa kupoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Al Hilal kumewaongezea morali katika maandalizi ya mchezo wa kesho ambao wanahitaji kushinda

"Tuko kwenye presha baada ya kupoteza mchezo wa kwanza, lakini imetupa nguvu ya kujiandaa vizuri kuelekea mchezo wa kesho"

"Tumekuja mapema kwa ajili ya kuzoea hali ya hewa. Hatuwezi kupanga matokeo ya mwisho yatakavyokuwa Lakini tunaweza kupanga jinsi tutakavyocheza ili kupata matokeo mazuri"

"Sio nzuri kucheza mechi bila mashabiki, binafsi napenda kuiona timu yangu ikicheza mbele ya mashabiki wengi, lakini kwa kesho tutawakosa mashabiki hapa uwanjani hivyo tuna jukumu la kupambana kuwapa furaha mashabiki wetu watakaokuwa nyumbani," alisema

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wenzake, Stephane Aziz Ki amesema wamejifunza kutoka kile kilichotokea katika mechi mbili zilizopita, kesho wanakwenda kupambana kusahihisha makosa

"Kila siku mpya uwanjani inatupa nafasi wachezaji ya kujifunza kitu kipya, mechi mbili zilizopita, ya Ligi ya Mabingwa na Ligi Kuu zimetupa funzo na kesho tutakwenda kupambana ili tupate matokeo mazuri," alisema Aziz Ki

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’