International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Disemba 07 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
7 Dec 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Disemba 07 2024

Wakala wa Alphonso Davies 'amekasirishwa' na jinsi Bayern Munich walivyofanya katika mazungumzo ya kusaini mkataba mpya wa beki huyo wa Canada mwenye umri wa miaka 24 na sasa anataka kusikiliza ofa kutoka Manchester United na Real Madrid , huku mikutano ikipangwa kufanyika Januari. (Bild)

Mawakala wa Manchester City wamemchagua kiungo wa kati wa Valencia na Uhispania Pepelu, 26, kama mtu anayefaa kuchukua nafasi ya Rodri, mwenye umri wa miaka 28, huku akiuguza jeraha. (Football Transfers)

Tyler Dibling wa Southampton anatazamwa na Manchester United na Aston Villa , na kiungo huyo wa kati wa Uingereza mwenye umri wa miaka 18 pia anaaminika kuwa kwenye rada za vilabu vya Ujerumani na Italia. (Sun)

Crystal Palace hawana uwezekano wa kupokea ofa kutoka kwa Manchester City na Arsenal kumusu kiungo wa kati wa Uingereza Adam Wharton, 20. (Football Insider)

Mkufunzi mpya wa Leicester City Ruud van Nistelrooy anatazamiwa kutoa ofa ya mkopo kwa kiungo wa kati wa zamani wa klabu ya Manchester United Toby Collyer mwenye umri wa miaka 20. (Sun)

Celtic wanaweza kutafuta kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Muingereza Carney Chukwuemeka kwa mkopo mwezi Januari. (Football Insider)

Mchezaji wa Bayern Munich Leroy Sane anaweza kupatikana kwa uhamisho wa bila malipo msimu ujao kwa vile 'kumekuwa na mafanikio kidogo' katika mazungumzo kuhusu kandarasi mpya kwa winga huyo wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 28. (Sky Sport Germany - in German)

Barcelona wamejiweka katika nafasi nzuri katika kinyang'anyiro cha kumsajili Jonathan Tah, ambaye mkataba wake unamalizika Bayer Leverkusen msimu ujao wa kiangazi, baada ya kukutana na mawakala wa beki huyo wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 28 wiki hii. (Mundo Deportivo - in Spanish)

Barcelona pia inawafuatilia mshambuliaji wa Sporting na Uswidi Viktor Gyokeres, 26, na mshambuliaji wa Lille ya Canada Jonathan David, 24, wakati wakipanga kuchukua nafasi ya mshambuliaji wa Poland Robert Lewandowski, 36. (AS - in Spanish)

Manchester City waliwahi kutuma ofa ya pauni milioni 35 kwa Barcelona kwa ajili ya kumnunua mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi kimakosa, muda mfupi baada ya klabu hiyo kuchukuliwa na Sheikh Mansour mwaka wa 2008. (Star)

Mkufunzi wa Ipswich Kieran McKenna ndiye chaguo la kwanza la Tottenham ikiwa Spurs itaamua kumfuta kazi meneja wa sasa Ange Postecoglou. (Football Transfers)

BBC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
9h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
21h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’