Yanga yapoteza tena Algeria

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th December 2024


Yanga yapoteza tena Algeria

Yanga imeacha alama nyingine tatu Algeria baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya MC Alger

Vijana wa kocha Saed Ramovic walicheza kwa nidhamu kubwa kwenye kipindi cha kwanza na kwenda mapumziko bila kuruhusu bao

Hata hivyo mambo hayakuwa mazuri upande wao katika kipindi cha pili baada Ayoub Abdelloui akifunga kwa kichwa dakika ya 64 baada ya walinzi wa Yanga kuzembea kuondoa mpira wa adhabu

Kuingia kwa bao hilo ni kama kuliiamsha Yanga iliyoanza kupeleka mashambulizi langoni kwa MC Alger lakini bado Alger waliendelea kuwa hatari kupitia mashambulizi ya kushitukiza

Mlinda lango Djigui Diarra akafanya makosa dakika za lala salama baada ya kutokea mpira ambao hakufanikiwa kuucheza na kuwapa nafasi Alger kufunga bao la pili

Ni alama nyingine tatu zinapotea ikiwa mechi ya pili Yanga inapoteza katika michuano ya ligi ya mabingwa

Mchezo unaofuata Yanga inakwenda tena ugenini kumenyana na TP Mazembe, Disemba 14

Bado kimahesabu Yanga ina nafasi ya kufanya vizuri ikiwa itashinda mechi mbili zilizobaki nyumbani na pia kufanya vizuri katika mechi nyingine mbili zilizobaki ugenini dhidi ya TP Mazembe na Al Hilal


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.