Local,Normal News,Yanga

Yanga yapoteza tena Algeria

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Dec 2024
Yanga yapoteza tena Algeria

Yanga imeacha alama nyingine tatu Algeria baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya MC Alger

Vijana wa kocha Saed Ramovic walicheza kwa nidhamu kubwa kwenye kipindi cha kwanza na kwenda mapumziko bila kuruhusu bao

Hata hivyo mambo hayakuwa mazuri upande wao katika kipindi cha pili baada Ayoub Abdelloui akifunga kwa kichwa dakika ya 64 baada ya walinzi wa Yanga kuzembea kuondoa mpira wa adhabu

Kuingia kwa bao hilo ni kama kuliiamsha Yanga iliyoanza kupeleka mashambulizi langoni kwa MC Alger lakini bado Alger waliendelea kuwa hatari kupitia mashambulizi ya kushitukiza

Mlinda lango Djigui Diarra akafanya makosa dakika za lala salama baada ya kutokea mpira ambao hakufanikiwa kuucheza na kuwapa nafasi Alger kufunga bao la pili

Ni alama nyingine tatu zinapotea ikiwa mechi ya pili Yanga inapoteza katika michuano ya ligi ya mabingwa

Mchezo unaofuata Yanga inakwenda tena ugenini kumenyana na TP Mazembe, Disemba 14

Bado kimahesabu Yanga ina nafasi ya kufanya vizuri ikiwa itashinda mechi mbili zilizobaki nyumbani na pia kufanya vizuri katika mechi nyingine mbili zilizobaki ugenini dhidi ya TP Mazembe na Al Hilal

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
4h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
14h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
14h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
16h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’