International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya Jumapili Disemba 08 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Dec 2024
Tetesi za usajili Ulaya Jumapili Disemba 08 2024

Jose Mourinho amefutilia mbali uwezekano wa nyota wa Ureno wa Al-Nassr Cristiano Ronaldo, 39, kujiunga naye Fenerbahce, akisema timu yake tayari ina washambuliaji watatu wazuri. (Goal)

William Saliba yuko tayari kuweka mustakabali wake wa muda mrefu kwa Arsenal licha ya beki huyo wa kati wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 23 kuwa mlengwa namba moja wa Real Madrid. (Sun)

West Ham itamfikiria kocha wa Middlesbrough Michael Carrick iwapo watamtimua meneja wa sasa Julen Lopetegui. (Daily Mirror)

Arsenal wanatazamiwa kukataa ofa za Januari kwa beki wa kati wa Poland Jakub Kiwior huku Napoli, AC Milan na Juventus zikimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24. (Daily Mirror)

Meneja wa Crystal Palace Oliver Glasner amefutilia mbali uwezekano wa kumrudisha fowadi Mfaransa Odsonne Edouard, 26, kutoka Leicester anakocheza kwa mkopo. (Talksport)

Mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 25, ambaye yuko kwa mkopo Galatasaray, ana nia ya kuungana na mkurugenzi wa zamani wa michezo wa klabu hiyo Cristiano Giuntoli, Juventus. (Il Mattino)

Mlinzi wa Manchester United na Argentina Lisandro Martinez, 26, yuko kwenye rada za Real Madrid huku mabingwa hao wa Ulaya wakitathmini uwezekano wa mabeki wapya wa kati. (TBR Football)

West Ham wanafikiria kumnunua mlinzi wa Chelsea Tosin Adarabioyo kwa mkopo Januari 27. (Footmercato)

Chelsea na Arsenal ziko mbioni kumsajili beki wa Brazil mwenye umri wa miaka 19 Vitor Reis kutoka Palmeiras. (Florian Plettenberg)

Paris St-Germain wanafikiria kumnasa mshambuliaji wa Sporting raia wa Sweden Viktor Gyokeres, huku Arsenal, Chelsea na Manchester United pia wakimtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (Fichajes)

BBC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
1h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
11h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’