Singida BS iko busy dirisha dogo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 9th December 2024


Singida BS iko busy dirisha dogo

Kuelekea dirisha dogo la usajili ambalo litafunguliwa wiki ijayo, Singida Black Stars imewarejesha wachezaji wake watatu waliokuwa wakiitumikia Tabora United kwa mkopo

Kiungo Morice Chukwu na walinzi wa kati Faria Ondongo na Hernest Malonga wote wamerejeshwa kunako klabu hiyo yenye Makao yake makuu mkoani Singida

Singida BS pia imewatoa wachezaji wengine watatu kwa mkopo kuzitumikia klabu nyingine za ligi kuu

Mlinzi wa kushoto Hamad Majimengi atajiunga na Pamba Jiji kama ilivyo kwa Habib Kyombo huku Kelvin Nashon akitua klabu ya Yanga

Singida BS pia inahusishwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji raia wa Ghana Jonathan Sowah aliyewahi kuitumikia Medeama Fc ya Ghana kabla ya kutimkia ligi kuu ya Libya


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.