Kuelekea dirisha dogo la usajili ambalo litafunguliwa wiki ijayo, Singida Black Stars imewarejesha wachezaji wake watatu waliokuwa wakiitumikia Tabora United kwa mkopo
Kiungo Morice Chukwu na walinzi wa kati Faria Ondongo na Hernest Malonga wote wamerejeshwa kunako klabu hiyo yenye Makao yake makuu mkoani Singida
Singida BS pia imewatoa wachezaji wengine watatu kwa mkopo kuzitumikia klabu nyingine za ligi kuu
Mlinzi wa kushoto Hamad Majimengi atajiunga na Pamba Jiji kama ilivyo kwa Habib Kyombo huku Kelvin Nashon akitua klabu ya Yanga
Singida BS pia inahusishwa kukamilisha usajili wa mshambuliaji raia wa Ghana Jonathan Sowah aliyewahi kuitumikia Medeama Fc ya Ghana kabla ya kutimkia ligi kuu ya Libya



