Local,Normal News,Yanga

Yanga ina mlima mrefu CAF CL

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Dec 2024
Yanga ina mlima mrefu CAF CL

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya ligi ya mabingwa (CAF CL) Yanga wana kazi ya kufanya ili kuweza kutinga robo fainali ya michuano hiyo baada ya kuanza hatua ya makundi kwa kusuasua

Baada ya juzi kupoteza mchezo wa pili mfululizo kwa kufungwa mabao 2-0 na MC Alger, Yanga imeendelea kushika nafasi ya nne kundi A ikiwa haina pointi

Vinara wa kundi hilo Al Hilal jana walipata ushindi mwingine wa mabao 2-1 dhidi ya TP Mazembe na hivyo kufikisha alama 6

MC Alger wanashika nafasi ya pili wakiwa na alama nne huku TP Mazembe wakiwa wa tatu na alama 1

Kila timu imesalia na mechi nne, hivyo licha kutokuwa na pointi mpaka sasa bado Yanga ina nafasi ya kusonga mbele hatua inayofuata kama itafanya vizuri katika mechi hizo zilizobaki

Mechi mbili dhidi ya TP Mazembe na MC Alger watacheza nyumbani huku mechi nyingine mbili dhidi ya Mazembe na Al Hilal watacheza ugenini

Mchezo unaofuata Yanga itasafiri Lubumbashi DR Congo kuikabili Mazembe kabla ya timu hizo kurudiana wiki mbili baadae jijini Dar es salaam

Yanga inahitaji kushinda angalau mechi tatu ili kuwa na nafasi ya kutinga robo fainali

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’