Yanga ina mlima mrefu CAF CL

Joel JJ By Joel JJ β€’ 9th December 2024


Yanga ina mlima mrefu CAF CL

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya ligi ya mabingwa (CAF CL) Yanga wana kazi ya kufanya ili kuweza kutinga robo fainali ya michuano hiyo baada ya kuanza hatua ya makundi kwa kusuasua

Baada ya juzi kupoteza mchezo wa pili mfululizo kwa kufungwa mabao 2-0 na MC Alger, Yanga imeendelea kushika nafasi ya nne kundi A ikiwa haina pointi

Vinara wa kundi hilo Al Hilal jana walipata ushindi mwingine wa mabao 2-1 dhidi ya TP Mazembe na hivyo kufikisha alama 6

MC Alger wanashika nafasi ya pili wakiwa na alama nne huku TP Mazembe wakiwa wa tatu na alama 1

Kila timu imesalia na mechi nne, hivyo licha kutokuwa na pointi mpaka sasa bado Yanga ina nafasi ya kusonga mbele hatua inayofuata kama itafanya vizuri katika mechi hizo zilizobaki

Mechi mbili dhidi ya TP Mazembe na MC Alger watacheza nyumbani huku mechi nyingine mbili dhidi ya Mazembe na Al Hilal watacheza ugenini

Mchezo unaofuata Yanga itasafiri Lubumbashi DR Congo kuikabili Mazembe kabla ya timu hizo kurudiana wiki mbili baadae jijini Dar es salaam

Yanga inahitaji kushinda angalau mechi tatu ili kuwa na nafasi ya kutinga robo fainali


  

More Stories

Yanga yarejea kileleni Ligi Kuu ikiibamiza Fountain Gate 2-0
Yanga yarejea kileleni Ligi Kuu ikiibamiza Fountain Gate 2-0
Today, READ MORE β†’
Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia
Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Simba yalimwa faini 10M, Mabena, Komba wakumbana na rungu la kamati ya saa 72
Simba yalimwa faini 10M, Mabena, Komba wakumbana na rungu la kamati ya saa 72
Today, READ MORE β†’
Simba yamfuatilia kipa wa Zimbabwe Nelson Chadya
Simba yamfuatilia kipa wa Zimbabwe Nelson Chadya
Today, READ MORE β†’
Zwane kukosa mechi zilizobaki kombe la Dunia
Zwane kukosa mechi zilizobaki kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Sowah kurejea Singida BS?
Sowah kurejea Singida BS?
Today, READ MORE β†’
Mubiru atua Azam Fc
Mubiru atua Azam Fc
Today, READ MORE β†’
Ligi Kuu: Yanga mikononi mwa Fountain Gate, mechi tatu kupigwa leo
Ligi Kuu: Yanga mikononi mwa Fountain Gate, mechi tatu kupigwa leo
Today, READ MORE β†’
Ghana yaandikisha ushindi wa pili kwa Afrika, Uingereza yaanza kwa kishindo
Ghana yaandikisha ushindi wa pili kwa Afrika, Uingereza yaanza kwa kishindo
Today, READ MORE β†’
DR Congo yapata sare ya kihistoria kombe la Dunia
DR Congo yapata sare ya kihistoria kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’