Simba, CS Sfaxien zatua pamoja Dar

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th December 2024


Simba, CS Sfaxien zatua pamoja Dar

Klabu ya Simba imerejea nchini Alfajiri ya leo Jumanne wakitokea Algeria katika mchezo wa raundi ya pili hatua ya makundi kombe la Shirikisho dhidi ya CS Constantine ambao walipoteza kwa kufungwa mabao 2-1

Wakati Simba ikitua, wapinzani wao katika kundi A, CS Sfaxien ya Tunisia nayo imetua nchini alfajiri kuelekea mchezo wa raundi ya tatu dhidi ya Simba

Ni Jumapili Disemba 15 katika uwanja wa Benjamin Mkapa Simba na CS Sfaxien zitaumana mechi ya kusaka tiketi ya kutinga robo fainali

CS SFaxien wametokea Angola ambako juzi walichapwa mabao 3-2 dhidi ya Bravos. Watunisia hao wamepoteza mechi zote mbili za kwanza wakiburuza mkia kundi A

Ni wazi wameuchukulia mchezo huo dhidi ya Simba kwa umuhimu mkubwa pengine ndio sababu wamekuja nchini mapema

Hata hivyo watahitaji kufanya kazi ya ziada kuchukua alama mbele ya Simba ambayo pia imetoka kupoteza mchezo kule Algeria

Simba inazihitaji alama tatu za mchezo huo ili kuweka hai mkakati wao wa kufuzu robo fainali


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.