Simba, CS Sfaxien zatua pamoja Dar

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th December 2024


Simba, CS Sfaxien zatua pamoja Dar

Klabu ya Simba imerejea nchini Alfajiri ya leo Jumanne wakitokea Algeria katika mchezo wa raundi ya pili hatua ya makundi kombe la Shirikisho dhidi ya CS Constantine ambao walipoteza kwa kufungwa mabao 2-1

Wakati Simba ikitua, wapinzani wao katika kundi A, CS Sfaxien ya Tunisia nayo imetua nchini alfajiri kuelekea mchezo wa raundi ya tatu dhidi ya Simba

Ni Jumapili Disemba 15 katika uwanja wa Benjamin Mkapa Simba na CS Sfaxien zitaumana mechi ya kusaka tiketi ya kutinga robo fainali

CS SFaxien wametokea Angola ambako juzi walichapwa mabao 3-2 dhidi ya Bravos. Watunisia hao wamepoteza mechi zote mbili za kwanza wakiburuza mkia kundi A

Ni wazi wameuchukulia mchezo huo dhidi ya Simba kwa umuhimu mkubwa pengine ndio sababu wamekuja nchini mapema

Hata hivyo watahitaji kufanya kazi ya ziada kuchukua alama mbele ya Simba ambayo pia imetoka kupoteza mchezo kule Algeria

Simba inazihitaji alama tatu za mchezo huo ili kuweka hai mkakati wao wa kufuzu robo fainali


  

More Stories

Yanga yarejea kileleni Ligi Kuu ikiibamiza Fountain Gate 2-0
Yanga yarejea kileleni Ligi Kuu ikiibamiza Fountain Gate 2-0
Today, READ MORE β†’
Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia
Kane aifikia rekodi ya Lineker ya mabao 10 kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Simba yalimwa faini 10M, Mabena, Komba wakumbana na rungu la kamati ya saa 72
Simba yalimwa faini 10M, Mabena, Komba wakumbana na rungu la kamati ya saa 72
Today, READ MORE β†’
Simba yamfuatilia kipa wa Zimbabwe Nelson Chadya
Simba yamfuatilia kipa wa Zimbabwe Nelson Chadya
Today, READ MORE β†’
Zwane kukosa mechi zilizobaki kombe la Dunia
Zwane kukosa mechi zilizobaki kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’
Sowah kurejea Singida BS?
Sowah kurejea Singida BS?
Today, READ MORE β†’
Mubiru atua Azam Fc
Mubiru atua Azam Fc
Today, READ MORE β†’
Ligi Kuu: Yanga mikononi mwa Fountain Gate, mechi tatu kupigwa leo
Ligi Kuu: Yanga mikononi mwa Fountain Gate, mechi tatu kupigwa leo
Today, READ MORE β†’
Ghana yaandikisha ushindi wa pili kwa Afrika, Uingereza yaanza kwa kishindo
Ghana yaandikisha ushindi wa pili kwa Afrika, Uingereza yaanza kwa kishindo
Today, READ MORE β†’
DR Congo yapata sare ya kihistoria kombe la Dunia
DR Congo yapata sare ya kihistoria kombe la Dunia
Today, READ MORE β†’