Klabu ya Coastal Union imefikia makubaliano ya pande zote mbili na aliyekuwa golikipa wao Ley Ngumbi Matamp ya kuvunja mkataba
Kupitia ukurasa rasmi wa klabu hiyo imethibitisha kufikiwa kwa makubaliano hayo
"Tumefikia makubaliano baina ya klabu yetu na golikipa wetu Ley Ngumbi Matamp ya kumaliza huduma za pande zote mbili"
"Uzoefu wako umechangia kwa asilimia kubwa mafanikio yetu ya msimu uliopita. Shukrani za kipekee kwa kocha wetu wa magolikipa Mansour Ally ambaye alitumia nguvu na maarifa makubwa ya kurudisha uwezo na kiwango chako ukawa msaada mkubwa eneo la kulinda lango letu"
"Tunakutakia kheri nyingi,na mafanikio zaidi katika maisha yako," ilimaliza taarifa ya Coastal Union
Matampi alijiunga Coastal Union msimu uliopita 2023/2024 akiwa mchezaji huru baada ya kumalizana na FC Lupopo ya Congo, na msimu huo aliibuka kuwa kipa bora wa msimu.



