International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya Jumatano, Disemba 11 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Dec 2024
Tetesi za usajili Ulaya Jumatano, Disemba 11 2024

Manchester United inataka kumuuza mshambuliaji wa Uingereza Marcus Rashford, 27, katika dirisha la uhamisho la Januari. (Sky Sport Germany)

United walikuwa tayari kumuuza Rashford aliyehitimu katika akademia yao msimu uliopita na sasa wanapokea ofa mpya. (Telegraph – Subscription Required)

The Red Devils pia wanaweza kumuuza Lisandro Martinez ikiwa Real Madrid itaongeza nia yao ya kumnunua beki huyo wa Argentina, 26. (Talksport)

Arsenal wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Serbia mwenye umri wa miaka 24 Dusan Vlahovic kutoka Juventus Januari. (TeamTalk)

Beki wa kati wa Uholanzi Virgil van Dijk, 33, yuko tayari kusaini mkataba mpya na Liverpool licha ya kukataa ofa ya awali. (Football Insider)

&Newcastle United inamfuatilia winga wa PSV Eindhoven wa Ubelgiji Johan Bakayoko, 21, kabla ya dirisha la uhamisho la Januari. (Telegraph – Subscription Required)

Barcelona wanaweza tu kumsajili Dani Olmo msimu wa ujao kucheza La Liga hadi Disemba 31, lakini fowadi huyo wa Uhispania, 26, atakuwa mchezaji huru ikiwa Barca hawatamsajili tena Januari. (Mundo Deportivo – In Spanish)

Arsenal wana hamu ya kumsajili Dan Ashworth kama mkurugenzi wao mpya wa michezo baada ya kuondoka Manchester United. (ESPN) Mazungumzo ya Liverpool kuhusu mkataba mpya na mshambuliaji wa Misri Mohamed Salah, 32, yanaendelea huku pande hizo mbili zikikaribia kuafikiana kuhusu muundo mpya wa malipo. (Sky Sports)

AC Milan wako tayari kumruhusu nahodha Theo Hernandez kuondoka katika klabu hiyo lakini watadai ada ya takriban £41m kwa beki huyo wa kushoto wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 27. (Calciomercato - Itali)

Chelsea haitafikiria kumruhusu mlinzi wa kati Tosin Adarabioyo mwenye umri wa miaka 27 kuondoka kwa mkopo mwezi Januari huku kukiwa na taarifa za yeye kutaka kuelekea West Ham. (Football Insider)

Kiungo wa kati wa Denmark Christian Eriksen, 32, anatarajiwa kuondoka Manchester United mwishoni mwa msimu huu. (Fabrizio Romano) Aston Villa wanafikiria kumwita Louie Barry, 21, kutoka kwa mkopo katika League One Stockport County ili kumpeleka mshambuliaji huyo wa Uingereza mwenye mabao 14 kwa klabu iliyo katika kiwango cha juu zaidi. (TeamTalk)

BBC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
3h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
7h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
13h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
13h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
13h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
15h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
19h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’