Local,Transfer News,Yanga, Singida

Yanga yamtambulisha Mwenda

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Dec 2024
Yanga yamtambulisha Mwenda

Siku tano kabla ya dirisha dogo la usajili kufunguliwa, Yanga imeanza kutambulisha silaha zake mpya baada ya mabingwa hao wa Tanzania Bara kutambulisha usajili wa mlinzi wa pembeni Israel Mwenda

Mwenda ametua Yanga kwa mkopo wa hadi mwishoni mwa msimu akitokea klabu ya Singida Black Stars

Beki huyo mwenye umri wa miaka 24, anamudu kucheza nafasi zote za ulinzi wa pembeni kulia na kushoto

Kabla ya kusajiliwa na Singida Black Stars mwanzoni mwa msimu huu, Mwenda alizitumikia klabu za KMC na Simba mara kadhaa akipata nafasi ya kuitwa timu ya Taifa

Yanga inakabiliwa na changamoto katika safu ya ulinzi hasa upande wa kushoto ambapo beki tegemeo Chadrack Boka anakabiliwa na majeraha ya mara kwa mara

Mbadala wake Nickson Kibabage hajaonyesha ushawishi wa kutosha kuaminiwa katika nafasi hiyo huku Kibwana Shomari akikosekana kwenye kikosi cha kwanza kwa muda mrefu kwa kilichoelezwa kupungua makali yake

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
4m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
3h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
5h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
9h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
10h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
12h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
15h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
22h ago
READ MORE β†’