Local,Transfer News,Simba

Mpanzu kuongezwa kikosi cha Simba CAF

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Dec 2024
Mpanzu kuongezwa kikosi cha Simba CAF

Kiungo mshambuliaji wa Simba Elie Mpanzu ataanza kuwatumikia Wekundu hao wa Msimbazi katika michuano ya kombe la Shirikisho la CAF (CAF CC) baada ya Januari 1 2025

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali ametoa ufafanuzi kuwa dirisha dogo la usajili la CAF litafunguliwa Januari 01 na kufungwa Januari 31 2025 wakati dirisha dogo la TFF likifunguliwa Disemba 16 na kufungwa Januari 15 2025

Hivyo Mpanzu ataanza kuitumikia Simba kwenye ligi ya ndani kuanzia wiki ijayo baada dirisha la TFF kufunguliwa lakini atalazimika kusubiri Januari 1 ili asajiliwe katika kikosi cha Simba kinachoshiriki kombe la Shirikisho

"Disemba 15 litafunguliwa dirisha ndogo la usajili wa ndani na Ellie Mpanzu atasajiliwa hapo kwa maana hiyo mechi yoyote ya ndani baada ya tarehe 15 atakuwa sehemu ya kikosi lakini dirisha la CAF ni mpaka Januari, 2025 kwahiyo mechi yoyote ya kimataifa kuanzia Januari atakuwa sehemu ya kikosi," alisema Ahmed

Disemba 18 Simba itacheza mechi ya ligi kuu dhidi ya KenGold ambayo itapigwa uwanja wa KMC Complex, huenda ikawa mechi ya kwanza kwa Mpanzu kuitumikia Simba

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
58m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’