Mpanzu kuongezwa kikosi cha Simba CAF

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th December 2024


Mpanzu kuongezwa kikosi cha Simba CAF

Kiungo mshambuliaji wa Simba Elie Mpanzu ataanza kuwatumikia Wekundu hao wa Msimbazi katika michuano ya kombe la Shirikisho la CAF (CAF CC) baada ya Januari 1 2025

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali ametoa ufafanuzi kuwa dirisha dogo la usajili la CAF litafunguliwa Januari 01 na kufungwa Januari 31 2025 wakati dirisha dogo la TFF likifunguliwa Disemba 16 na kufungwa Januari 15 2025

Hivyo Mpanzu ataanza kuitumikia Simba kwenye ligi ya ndani kuanzia wiki ijayo baada dirisha la TFF kufunguliwa lakini atalazimika kusubiri Januari 1 ili asajiliwe katika kikosi cha Simba kinachoshiriki kombe la Shirikisho

"Disemba 15 litafunguliwa dirisha ndogo la usajili wa ndani na Ellie Mpanzu atasajiliwa hapo kwa maana hiyo mechi yoyote ya ndani baada ya tarehe 15 atakuwa sehemu ya kikosi lakini dirisha la CAF ni mpaka Januari, 2025 kwahiyo mechi yoyote ya kimataifa kuanzia Januari atakuwa sehemu ya kikosi," alisema Ahmed

Disemba 18 Simba itacheza mechi ya ligi kuu dhidi ya KenGold ambayo itapigwa uwanja wa KMC Complex, huenda ikawa mechi ya kwanza kwa Mpanzu kuitumikia Simba


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.