International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jummosi, Disemba 14 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Dec 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Jummosi, Disemba 14 2024

Kiungo wa kati wa Bayer Leverkusen na Ujerumani Florian Wirtz, 21, na kiungo wa kati wa Newcastle wa Brazil Bruno Guimaraes, 27, wanafuatiliwa na Manchester City. (Times - subscription required)

Kocha wa Man City Pep Guardiola pia atapata uungwaji mkono kumsajili kiungo wa kati wa Real Sociedad na Uhispania Martin Zubimendi mwenye umri wa miaka 25. (ESPN)

Chelsea na Liverpool wanatazamiwa kumwinda mlinzi Milos Kerkez, 21, lakini Bournemouth watafanya kila wawezalo kumbakisha mchezaji huyo wa kimataifa wa Serbia. (Football Insider)

Mikel Arteta anataka kumuongeza mlinzi wa Juventus na Serbia Dusan Vlahovic, 24, kwenye kikosi chake cha Arsenal mwezi Januari. (Caught Offside)

Real Madrid wamejiondoa kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili mlinzi wa AC Milan Theo Hernandez, 27, na kurahisisha kazi kwa Manchester United wanaomtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa. (Fichajes - in Spanish)

Gary O'Neil ana mechi ya Jumamosi dhidi ya Ipswich Town ili kuokoa kazi yake kama kocha wa Wolves. (Football Insider)

Bournemouth wanataka meneja Andoni Iraola atie saini mkataba mpya kutokana na hofu kwamba klabu nyingine za Ligi ya Primia zinaweza kumlenga Mhispania huyo. (TBR Football)

RB Leipzig wanataka kumsajili mshambuliaji wa Uholanzi wa Paris St-Germain Xavi Simons, 21, kwa mkataba wa kudumu, lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Liverpool. (Caught Offside)

Manchester United wamefikia makubaliano ya mdomo na Cerro Porteno kumnunua beki wa pembeni wa Paraguay, Diego Leon, 17. (Fabrizio Romano)

Kiungo wa kati wa Denmark Christian Eriksen, 32, anaweza kuuzwa na Manchester United mwezi Januari iwapo kutapatikana ofa ya kuvutia. (Florian Plettenberg)

Everton wanapanga kumnunua winga wa Lyon na Ghana Ernest Nuamah, 21, mwezi Januari. (Football Insider)

Kundi linaloongozwa na Dan Friedkin linakaribia kufikia makubaliano ya kuinunua Everton, huku ununuzi ukikamilika wiki ijayo. (Times - subscription required) Kocha wa Everton Sean Dyche hatarajiwi kufutwa kazi mara moja baada ya Kundi la Friedkin kununua klabu hiyo. (Football Insider)

Tottenham hawana mpango wa kuchagua kumsajili kwa mkopo kwa mkataba wa kudumu mshambuliaji wa Ujerumani Timo Werner, 28, kutoka RB Leipzig mwishoni mwa msimu. (GiveMeSport)

BBC

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
12h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’