Local,Normal News,Simba, Sfaxien

Simba dimbani dhidi ya CS Sfaxien CAF CC leo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Dec 2024
Simba dimbani dhidi ya CS Sfaxien CAF CC leo

Mikiki mikiki ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC) inaendelea leo ambapo Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc watakuwa uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili CS Sfaxien kutoka Tunisia

Mechi muhimu kwa Simba kubeba alama zote tatu leo ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu hatua ya robo fainali

Simba inayoshika nafasi ya pili kundi A, ilipoteza mchezo uliopita dhidi ya CS Constantine uliopigwa Algeria, leo ni matokeo ya aina moja tu ambayo mashabiki wa Simba wanayatarajia, USHINDI

Licha ya kupoteza mechi zao mbili, CS Sfaxien sio timu nyepesi na bila shaka leo huenda wakatoa upinzani mkali kwa Simba

Timu hiyo ilitua nchini mapema ambapo wako katika ardhi ya Tanzania kwa takribani siku sita

Walisafiri moja kwa moja kutoka Angola kuja Tanzania baada ya mchezo dhidi ya Bravos ambao walipoteza kwa mabao 3-2 Jumapili iliyopita

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema leo vijana wake watakuwa tofauti kimbinu ukilinganisha na mechi yao iliyopita ambayo walikuwa ugenini

Simba leo inatarajiwa kucheza soka la kushambulia zaidi huku wakichukua tahadhari ya mashambulizi ya kushitukiza ya Sfaxien

Mchezo unatarajiwa kupigwa kuanzia saa 10 jioni..

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
3h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
13h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
13h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
15h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’