Simba dimbani dhidi ya CS Sfaxien CAF CC leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th December 2024


Simba dimbani dhidi ya CS Sfaxien CAF CC leo

Mikiki mikiki ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC) inaendelea leo ambapo Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc watakuwa uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili CS Sfaxien kutoka Tunisia

Mechi muhimu kwa Simba kubeba alama zote tatu leo ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu hatua ya robo fainali

Simba inayoshika nafasi ya pili kundi A, ilipoteza mchezo uliopita dhidi ya CS Constantine uliopigwa Algeria, leo ni matokeo ya aina moja tu ambayo mashabiki wa Simba wanayatarajia, USHINDI

Licha ya kupoteza mechi zao mbili, CS Sfaxien sio timu nyepesi na bila shaka leo huenda wakatoa upinzani mkali kwa Simba

Timu hiyo ilitua nchini mapema ambapo wako katika ardhi ya Tanzania kwa takribani siku sita

Walisafiri moja kwa moja kutoka Angola kuja Tanzania baada ya mchezo dhidi ya Bravos ambao walipoteza kwa mabao 3-2 Jumapili iliyopita

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema leo vijana wake watakuwa tofauti kimbinu ukilinganisha na mechi yao iliyopita ambayo walikuwa ugenini

Simba leo inatarajiwa kucheza soka la kushambulia zaidi huku wakichukua tahadhari ya mashambulizi ya kushitukiza ya Sfaxien

Mchezo unatarajiwa kupigwa kuanzia saa 10 jioni..


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.