Mikiki mikiki ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC) inaendelea leo ambapo Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc watakuwa uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili CS Sfaxien kutoka Tunisia
Mechi muhimu kwa Simba kubeba alama zote tatu leo ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu hatua ya robo fainali
Simba inayoshika nafasi ya pili kundi A, ilipoteza mchezo uliopita dhidi ya CS Constantine uliopigwa Algeria, leo ni matokeo ya aina moja tu ambayo mashabiki wa Simba wanayatarajia, USHINDI
Licha ya kupoteza mechi zao mbili, CS Sfaxien sio timu nyepesi na bila shaka leo huenda wakatoa upinzani mkali kwa Simba
Timu hiyo ilitua nchini mapema ambapo wako katika ardhi ya Tanzania kwa takribani siku sita
Walisafiri moja kwa moja kutoka Angola kuja Tanzania baada ya mchezo dhidi ya Bravos ambao walipoteza kwa mabao 3-2 Jumapili iliyopita
Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema leo vijana wake watakuwa tofauti kimbinu ukilinganisha na mechi yao iliyopita ambayo walikuwa ugenini
Simba leo inatarajiwa kucheza soka la kushambulia zaidi huku wakichukua tahadhari ya mashambulizi ya kushitukiza ya Sfaxien
Mchezo unatarajiwa kupigwa kuanzia saa 10 jioni..



