Mnyama amebeba alama zote tatu uwanja wa Benjamin Mkapa akiondoka na ushindi wa mabao 2-1 katika mechi muhimu ya hatua ya makundi kombe la Shirikisho dhidi ya CS Sfaxien
Kibu Denis leo alikuwa shujaa wa Simba akifunga mabao yote mawili katika mchezo huo uliokuwa na presha kubwa
Makosa ya beki Che Malone Fondoh yaliinufaisha CS Sfaxien kufunga bao la mapema dakika ya pili tu
Hata hivyo Kibu Denis akairejesha Simba mchezoni dakika 8 baadae akimalizia mpira wa adhabu uliopigwa na Jean Ahoua
Simba ilishambulia muda wote wa mchezo, wakihamia langoni kwa Sfaxien kipindi cha pili lakini changamoto ilikuwa katika umaliziaji
Hatimaye dakika ya mwisho kabisa ya mchezo, Kibu akaweka bao kambani lililoihakikishia Simba alama tatu muhimu nyumbani
Simba imefikisha alama sita katika nafasi ya pili kundi A sawa na CS Constantine



