Kibu aibabe Simba kwa Mkapa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th December 2024


Kibu aibabe Simba kwa Mkapa

Mnyama amebeba alama zote tatu uwanja wa Benjamin Mkapa akiondoka na ushindi wa mabao 2-1 katika mechi muhimu ya hatua ya makundi kombe la Shirikisho dhidi ya CS Sfaxien

Kibu Denis leo alikuwa shujaa wa Simba akifunga mabao yote mawili katika mchezo huo uliokuwa na presha kubwa

Makosa ya beki Che Malone Fondoh yaliinufaisha CS Sfaxien kufunga bao la mapema dakika ya pili tu

Hata hivyo Kibu Denis akairejesha Simba mchezoni dakika 8 baadae akimalizia mpira wa adhabu uliopigwa na Jean Ahoua

Simba ilishambulia muda wote wa mchezo, wakihamia langoni kwa Sfaxien kipindi cha pili lakini changamoto ilikuwa katika umaliziaji

Hatimaye dakika ya mwisho kabisa ya mchezo, Kibu akaweka bao kambani lililoihakikishia Simba alama tatu muhimu nyumbani

Simba imefikisha alama sita katika nafasi ya pili kundi A sawa na CS Constantine


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.