Tabora United kuendelea kugawa dozi NBC PL leo?

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th December 2024


Tabora United kuendelea kugawa dozi NBC PL leo?

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mechi za raundi ya 15 zitaendelea katika viwanja viwili

Walina asali Tabora United watakuwa dimba la Ali Hassan Mwinyi kuikaribisha Coastal Union katika mchezo utakaopigwa saa 10 jioni

Tabora United wamekuja na utaratibu wa 'kurambisha' asali kila anayekanyaga dimba la Ali Hassan Mwinyi, je wataendeleza utaratibu huo mbele ya Coastal Union leo?

Azam Fc baada ya kupoteza mchezo uliopita dhidi ya Tabora United, watakuwa na nafasi ya kuendelea kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi pale watakapowakaribisha Fountain Gate dimba la Azam Complex, mchezo utakaopigwa saa 1 usiku


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.