Local,Normal News,KenGold, Simba

Kocha Simba apania ushindi dhidi ya KenGold

Joel JJ By Joel JJ
17 Dec 2024
Kocha Simba apania ushindi dhidi ya KenGold

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema licha ya ugumu wa ratiba inayowakabili mbele yao, kikosi chake kiko tayari kuwania alama tatu katika mchezo unaofuata ligi kuu ya NBC dhidi ya KenGold

Baada ya mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya CS Sfaxien ambao Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1, kesho tena Simba inashuka dimba la KMC Complex kuikabili KenGold 

Fadlu amesema baada ya kuwapa mapumziko wachezaji wake hapo jana, leo watakamilisha maandalizi kuelekea mchezo huo ambao wanazihitaji alama zote tatu

Fadlu amesema hawapaswi kuwadharau wapinzani wao licha ya nafasi waliyopo katika msimamo wa ligi kwani hawana cha kupoteza

"Tunakabiliwa naa ratiba ya kucheza mechi nne ndani ya muda mfupi lakini lazima tuwe tayari kwa ratiba hii"

"Baada ya mchezo dhidi ya CS Sfaxien, leo tutafanya maandalizi yetu ya mwisho kwa kuzingatia aina ya mpinzani tunayekwenda kucheza nae"

"Tunajua ubora wa KenGold, tunapaswa kucheza kwa tahadhari bila kuwapa nafasi ya kutushambulia kwa kushitukiza"

"Haitakuwa mechi nyepesi hivyo hatupaswi kufikiria tutakwenda uwanjani na kuchukua alama tatu tu, tutahitaji kupambana na muhimu zaidi ni kushinda mchezo huo", alisema Fadlu

Katika kipindi cha siku 10 Simba inatarajiwa kucheza mechi nne za ligi kuu. Mchezo utakaofuata baada ya KenGold ni dhidi ya Kagera Sugar utakaopigwa Disemba 21 uwanja wa Kaitaba, Kagera

Baada ya mchezo huo, Simba itarejea Dar kumenyana na JKT Tanzania Disemba 24 kisha kusafiri mkoani Singida kuikabili Singida BS, Disemba 28

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
58m ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE →