Fadlu apania ushindi wa kwanza Kaitaba

Joel JJ By Joel JJ • 20th December 2024


Fadlu apania ushindi wa kwanza Kaitaba

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema kikosi chake kimetua mkoani Kagera kikiwa kamili  kwa lengo la kubeba alama zote tatu katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar ambao utapigwa uwanja wa Kaitaba kesho Jumamosi

Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari kuelekea mchezo huo, Fadlu amesema misimu ya karibuni Simba haijapata ushindi katika uwanja wa Kaitba lakini sasa ni wakati wa kubadilisha rekodi hiyo

"Tumekuja hapa tukiwa na dhamira moja, kusaka ushindi katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar"

"Rekodi zinaonyesha hatua matokeo mazuri dhidi ya wapinzani wetu hasa wanapokuwa nyumbani katika misimu kadhaa iliyopita"

"Awamu hii tumekuja kivingine na maandalizi tuliyoyafanya tunaamini tutapata ushindi," alisema Fadlu

Katika misimu miwili ya 2022/23 na 2023/24 Simba iliondoka na alama moja Kaitaba ikilazimishwa sare ya bao 1-1 katika mechi zote mbili

Msimu huu mpaka sasa Simba imeweka rekodi ya kibabe katika mechi za ugenini, wakibeba alama tatu katika kila mechi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.