Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema kikosi chake kimetua mkoani Kagera kikiwa kamili kwa lengo la kubeba alama zote tatu katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar ambao utapigwa uwanja wa Kaitaba kesho Jumamosi
Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari kuelekea mchezo huo, Fadlu amesema misimu ya karibuni Simba haijapata ushindi katika uwanja wa Kaitba lakini sasa ni wakati wa kubadilisha rekodi hiyo
"Tumekuja hapa tukiwa na dhamira moja, kusaka ushindi katika mchezo dhidi ya Kagera Sugar"
"Rekodi zinaonyesha hatua matokeo mazuri dhidi ya wapinzani wetu hasa wanapokuwa nyumbani katika misimu kadhaa iliyopita"
"Awamu hii tumekuja kivingine na maandalizi tuliyoyafanya tunaamini tutapata ushindi," alisema Fadlu
Katika misimu miwili ya 2022/23 na 2023/24 Simba iliondoka na alama moja Kaitaba ikilazimishwa sare ya bao 1-1 katika mechi zote mbili
Msimu huu mpaka sasa Simba imeweka rekodi ya kibabe katika mechi za ugenini, wakibeba alama tatu katika kila mechi



