Local,Normal News,Yanga, Prisons

Yanga vs Prisons KMC Complex leo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Dec 2024
Yanga vs Prisons KMC Complex leo

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo ambapo mchezo mmoja utapigwa uwanja wa KMC Complex, Kinondoni jijini Dar es salaam

Mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga watakuwa na kibarua kizito mbele ya Tanzania Prisons katika mchezo utakaopigwa saa jioni

Ni mechi itakayokutanisha timu mbili zenye malengo tofauti. Yanga itakuwa ikisaka ushindi mnono ili isogee katika nafasi ya pili kwenye msimamo na kuendelea kuwapa presha watani zao Simba ambao jana walipata ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya Kagera Sugar

Tanzania Prisons imekusanya alama 11 katika mechi 14 ikishika nafasi ya 14, ni wazi watashuka katika dimba la KMC Complex leo kupambana kujiondoa katika eneo la hatari

Utakuwa mchezo wa tatu wa ligi kwa kocha mkuu wa Yanga Sead Ramovic ambaye amekusanya alama 6 kwa timu yake kushinda mechi mbili zilizopita

Aidha utakuwa mchezo wa pili kwa Yanga kucheza katika dimba la KMC Complex baada ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mashujaa Fc katika uwanja huo mshambuliaji Prince Dube akifungua akaunti yake ya mabao msimu huu akifunga hat-trik

Yanga inashika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi ikiwa na alama 30, ushindi wa kuanzia mabao matatu utawahakikishia Wananchi kusogea katika nafasi ya pili

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
58m ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
4h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
6h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
10h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
10h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
11h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
13h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
16h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
23h ago
READ MORE β†’