Local,Normal News,Yanga, Dodoma

Ramovic aihofia Dodoma Jiji

Joel JJ By Joel JJ
β€’
24 Dec 2024
Ramovic aihofia Dodoma Jiji

Kocha Mkuu wa Yanga Sead Ramovic amesema kikosi chake kiko tayari kwa mechi ngumu ya ligi kuu dhidi ya Dodoma Jiji ambayo itapigwa kesho Jumatano katika uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma

Akizungumza katika Mkutano na wanahabari, Ramovic alisema ameichambua Dodoma Jiji na kubaini ni timu ngumu hasa inapocheza katika uwanja wa Jamhuri hivyo watahitaji kucheza kwa tahadhari kubwa ili kupata alama 3

"Tumewatazama kwa makini sana Dodoma Jiji, wanacheza vizuri wakiwa nyumbani, tunafahamu ni wagumu mno wanapocheza nyumbani hivyo tumeshajiandaa kukabiliana nao. Alama tatu kesho muhimu mno kwetu ili tuendelee kubaki kwenye mipango yetu"

"Ushindi katika mchezo huo unabeba dhima nzima ya kujitoa kwa kila namna, kama tusipojitoa kwa kila hali hapo kesho matarajio ya ushindi yatakuwa madogo"

"Kimsingi tumekuja hapa na tumeshajiandaa kisawasawa na tuna imani ya kuondoka alama tatu. Bila shaka mchezo umekaa kimtego kutokana na ratiba lakini hiyo haiondoi dhamira yetu ya kushinda," alisema Ramovic

Aidha kocha huyo raia wa Ujerumani amesema atalazima kufanya 'rotation' ya kikosi cha katika baadhi ya nafasi ili kuhakikisha anatunza nguvu ya kila mchezo kwa ajili ya mapambano katika mechi ambazo zinafuatana karibu karibu

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’