Local,Normal News,Yanga, Simba, Azam, Fountain Gate, Singida BS

Tanzania uhakika AFCON 2025, rufaa ya Guinea yakwama

Joel JJ By Joel JJ
β€’
27 Dec 2024
Tanzania uhakika AFCON 2025, rufaa ya Guinea yakwama

Kamati ya nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) imetupilia mbali rufaa ya Guinea dhidi ya Tanzania na hivyo kuipa uhakika Taifa Stars kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon 2025) nchini Morocco

Guinea ilikata rufaa hiyo baada ya mchezo namba 143 wa kuwania kufuzu Afcon baina yao na Tanzania uliochezwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, Novemba 19, 2024 ikiitaka kamati ya nidhamu ya CAF kuiondoa Tanzania katika fainali za Afcon 2025 wakidai ilifanya kosa la kufoji kinyume na kanuni

Kwa mujibu wa rufaa hiyo, Guinea ilidai kuwa mchezaji Ibrahim Ame wa Tanzania aliyeingia kipindi cha pili kwenye mechi hiyo ambayo Tanzania iliibuka na ushindi wa bao 1-0 alikuwa na namba tofauti kwenye jezi kulinganisha na ile iliyopo kwenye fomu ya orodha ya wachezaji wa kutumika kwenye mechi hiyo

Guinea waliiomba kamati ya nidhamu ya CAF kuiengua Tanzania na kisha nafasi ya kucheza Afcon 2025 wapewe wao

Hata hivyo kamati ya nidhamu ya CAF iliyoketi Desemba 19, mwaka huu imeamua kuwa matokeo ya mchezo huo yabaki kama ilivyokuwa na Tanzania ibaki na haki ya kushiriki Afcon 2025

Taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu la Guinea (Feguifoot), imeeleza kuwa rufaa yao imetupiliwa mbali

"Kamati ya nidhamu ya CAF imekubali kwamba uhifadhi wa ushahidi uliofanywa na Shirikisho la Soka Guinea wakati wa mechi namba 143, Tanzania vs Guinea unakubalika katika fomu"

"Hata hivyo umekataliwa kwa vile hakuna hoja ya msingi," imefafanua taarifa hiyo ya Shirikisho la Soka Guinea

Mapema baada ya kusambaa kwa taarifa za Guinea kukata rufaa, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) liliwatoa wasiwasi Watanzania kwa kufafanua kuwa taratibu zote zilifuatwa katika kumtumia Ibrahim Ame kwenye mchezo huo.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’