Ikangalombo asubiri utambulisho Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th January 2025


Ikangalombo asubiri utambulisho Yanga

Wakati Yanga ikiibamiza TP Mazembe mabao 3-1 katika nchezo wa ligi ya mabingwa uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa juzi, nyota anayesubiri utambulisho Jangwani Jonathan Ikangalombo alikuwa jukwaani akishuhudia mchezo huo

Ikangalombo alitua Tanzania mapema Jumamosi na moja kwa moja kuelekea uwanja wa Benjamin Mkapa kushuhudia mchezo huo

Imeelezwa kocha mkuu wa Yanga Sead Ramovic amepitisha usajili wa winga huyo aliyekuwa akiitumikia AS Vita akitajwa kuchukua nafasi ya Jean Baleke ambaye Yanga imesitisha mkataba wake wa mkopo na kumrejesha katika klabu yake, TP Mazembe

Awali Yanga ilitaka kusajili mshambuliajii lakini Ramovic aligomea mpango huyo akihitaji aletewe winga

Kocha huyo raia wa Ujerumani ni kama anataka kurejesha utamaduni wa Yanga kutengeneza mashambulizi yake kupitia mawinga na walinzi wa pembeni

Ramovic amekuwa akimtumia Mzize kama winga akitokea pembeni na kuingia kati. Mzize amepachika mabao 6 katika mashindano yote tangu ujio wa Ramovic

Ikangalombo ni winga mwenye kasi na uwezo mkubwa wa kupachika mabao akitokea pembeni kama afanyavyo Mzize sasa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.