Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania aliyekuwa akikipiga kunako ligi kuu ya nchini Zambia, Eliuter Mpepo , yuko mbioni kusaini mkataba kujiunga na Tabora United
Mbali na Tabora, mchezaji huyo amegeuka lulu kwenye Ligi Kuu ya NBC baada vilabu vingine kuingilia dili hilo wakiitaka saini yake
Mpepo amewahi kukipiga Mtibwa Sugar, Prisons, Singida United, Build Con na Trident zote za Zambia na Interclube ya Angola
Waajiri wake wa zamani, Tz Prisons wao wameenda mbali zaidi na tayari wapo kwenye mazungumzo na nyota huyo ili kuweza kuinasa saini yake



