Local,Normal News,Simba

Kocha Simba apania kufuzu robo fainali CAF CC kibabe

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Jan 2025
Kocha Simba apania kufuzu robo fainali CAF CC kibabe

Licha ya kikosi chake kuhitaji sare tu dhidi ya Bravos ili kutinga robo fainali ya kombe la Shirikisho (CAF CC), Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amesema wanakwenda Angola kwenda kusaka alama tatu

Mwishoni mwa wiki iliyopita, Simba iliandikisha ushindi wake wa kwanza ugenini msimu huu katika michuano ya kombe la Shirikisho (CAF CC) wakiichapa CS Sfaxien bao 1-0 katika mchezo uliopigwa Tunisia

Simba ilirejea jana kutoka Tunisia na wanatarajiwa kuondoka Dar mapema Alhamisi kuelekea Angola kwa ajili ya mchezo huo

Akizungumza muda mfupi baada ya kutua kutoka Tunisia, Fadlu alieleza furaha yake kwa vijana wake kupambana na kupata ushindi muhimu Tunisia

Fadlu alisema hesabu zao ni kushinda mchezo unaofuata ili kutinga robo fainali na kuhakikisha wanamaliza kwa ushindi mechi ya mwisho dhidi ya CS Constantine na kumaliza vinara wa kundi A

"Nina furaha baada ya kufanikiwa kupata ushindi ugenini Tunisia. CS Sfaxien ni moja kati ya timu kubwa barani Afrika, ina uzoefu, kwa hiyo haukuwa ushindi uliopatikana kirahisi"

"Uwanja pia haukuwa mzuri sana, lakini kikubwa tumepata matokeo ya ushindi. Kwa sasa tunahitaji sare ili tufuzu, ingawa hatutacheza ili kusaka sare, bali ushindi"

"Mechi ya mwisho tutataka tushinde ili tuongoze kundi, lakini haraka iwezekanavyo tunataka kufuzu kwenda robo, tutafanya kila linalowezekana lengo litimie," alisema Fadlu

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
43m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’