Prisons yachukua wawili Singida BS

Joel JJ By Joel JJ β€’ 9th January 2025


Prisons yachukua wawili Singida BS

Tanzania Prisons imeendelea kujiimarisha kuelekea mzunguuko wa pili ligi kuu ya NBC ambapo maafande hao wamefanikiwa kunasa nyota wawili kwa mkopo kutoka klabu ya Singida Black Stars

Kiungo wa ushambuliaji Rabbin Sanga ametua Tanzania Prisons kwa mkopo wa miezi sita akitokea Singida Black Stars

Rabbin aliwahi kuitumikia Fountain Gates katika timu za vijana na timu kubwa

Prisons pia imekamilisha usajili wa kiungo mkabaji Amade Momade (28) kwa mkopo wa miezi sita. Momade ni mchezaji wa timu ya Taifa ya Msumbiji


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.