Local,Normal News,Yanga, Hilal

Hatma ya Yanga mikononi mwa Al Hilal CAF CL leo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Jan 2025
Hatma ya Yanga mikononi mwa Al Hilal CAF CL leo

Mechi za raundi ya tano hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika zinaendelea kutimua vumbi leo Jumapili ambapo mabingwa wa Tanzania Bara Yanga wako ugenini kumenyana na Al Hilal huko Mauritania

Dakika za mchezo huo utakaopigwa saa 4 usiku zitaamua hatma ya Yanga kuendelea kuwania tiketi ya robo fainali au kuyaaga mashindano hayo

Leo Yanga inahitaji ushindi au hata matokeo ya sare ili kuendelea kubaki na matumaini ya kusonga mbele lakini kama itapoteza mchezo huo, basi itaaga rasmi mashindano

Al Hilal inayoongoza kundi A ikiwa na alama 10 tayari imekata tiketi ya robo fainali lakini katika mchezo huo inahitaji angalau alama 1 ili kujihakikishia kumaliza nafasi ya kwanza katika kundi

MC Alger itakuwa ikifuatilia kwa karibu mchezo huo kwani matokeo ya ushindi kwa Al Hilal yatawapa tiketi ya kutinga robo fainali na alama zao nane

Endapo Yanga itashinda itafikisha alama 7 na ili kufuzu itahitaji kushinda mechi ya mwisho dhidi ya MC Alger ambayo itapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa Januari 18

Lakini pia kama Yanga itapata sare leo, itakuwa bado na nafasi ya kutinga robo fainali kama itashinda kuanzia mabao 2-0 katika mchezo dhidi ya MC Alger

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’