Simba imefanikiwa kutinga robo fainali ya kombe la Shirikisho (CAF CC) baada ya kulazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya Bravos Fc katika mchezo uliopigwa huko Angola
Makosa ya beki Che Malone Fondoh yaliinufaisha Bravos kufunga bao la mapema hata hivyo Lionel Ateba aliisawzishia Simba katika kipindi cha pili bao ambalo limeihakikishia Simba kufuzu
Pengine ulikuwa mchezo ambao Simba ingeweza kuibuka na ushindi Kibu Denis akikosa nafasi tatu katika kipindi cha kwanza
Ulikuwa mchezo ambao Simba iliucheza kimkakati zaidi na hatimaye mpango wa kocha Fadlu Davids umekamilika



