Klabu ya KenGold iko katika hatua ya mwisho kukamilisha usajili wa kiungo mkabaji Zawadi Mauya kutoka klabu ya Singida Black Stars, imefahamika
Mazungumzo baina ya vilabu vya Singida Black Stars na Ken Gold juu ya mchezaji huyo yapo katika hatua za mwisho
Muda wowote kuanzia sasa usajili huo utakamilika, Mkataba wa Miezi Sita wa kuwatumikia Ken Gold pia wenye kipengele cha kuongeza zaidi endapo wataridhia huduma yake kwa msimu ujao
Mauya alijiunga na Singida BS msimu huu akitokea klabu ya Yanga aliyoitumikia kwa misimu minne
Hata hivyo kiungo wa zamani wa Kagera Sugar amekosa nafasi kwenye kikosi cha kwanza cha Singida BS



