Nyota wa zamani wa Taifa Stars, Mrisho Ngasa, ataungana na magwiji wengine wawili katika droo ya fainali za CHAN2024 itakayofanyika nchini Kenya Jumatano ya Januari 15
Wachezaji hao wa zamani wa soka ni Hassan Wasswa kutoka Uganda na Mkenya McDonald Mariga ambao wataungana na Mrisho Ngasa kutoka Tanzania
Droo hiyo itakayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Kenyatta, Nairobi Kenya, Jumatano saa 2:00 usiku
Michuano ya CHAN 2024 itaanza kutimua vumbi Februari 1, na kuhitimishwa Februari 28, 2025, katika mataifa ya Kenya, Uganda na Tanzania.
Droo hiyo itaruka LIVE AzamSports1HD kuanzia saa 2:00 usiku



