Ngasa, Mariga, Waswa kuendesha droo ya CHAN

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th January 2025


Ngasa, Mariga, Waswa kuendesha droo ya CHAN

Nyota wa zamani wa Taifa Stars, Mrisho Ngasa, ataungana na magwiji wengine wawili katika droo ya fainali za CHAN2024 itakayofanyika nchini Kenya Jumatano ya Januari 15

Wachezaji hao wa zamani wa soka ni Hassan Wasswa kutoka Uganda na Mkenya McDonald Mariga ambao wataungana na Mrisho Ngasa kutoka Tanzania

Droo hiyo itakayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Kenyatta, Nairobi Kenya, Jumatano saa 2:00 usiku

Michuano ya CHAN 2024 itaanza kutimua vumbi Februari 1, na kuhitimishwa Februari 28, 2025, katika mataifa ya Kenya, Uganda na Tanzania.

Droo hiyo itaruka LIVE AzamSports1HD kuanzia saa 2:00 usiku


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.