International,Transfer News,

Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne, Januari 14 2025

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Jan 2025
Tetesi za usajili Ulaya, Jumanne, Januari 14 2025

Manchester United wanasemekana kumthamini winga Alejandro Garnacho, 20, kwa takribani pauni milioni 42, huku kukiwa na nia ya Napoli kumnyakua mchezaji huyo (Sport Italia)

Bayern Munich wameungana na Chelsea katika mbio za kumnunua kiungo wa kati wa Manchester United na Uingereza Kobbie Mainoo, 19. (Sun)

Manchester City wako tayari kumruhusu mlinzi Kyle Walker, 34, kuondoka bila malipo mwezi huu huku AC Milan na Inter Milan wakionesha nia ya kumnasa mchezaji huyo. (Gazzetta dello Sport, nje)

AC Milan itamfuatilia rasmi mshambuliaji wa Manchester United Marcus Rashford, 27, ambaye anatazamiwa kuondoka Old Trafford mwezi huu. (Sky Sports)

Borussia Dortmund pia wameripotiwa kukutana na wawakilishi wa Rashford kwa matumaini ya kufikia mkataba wa Januari. (Sky Sport Ujerumani)

Aston Villa wamekubali mkataba wa pauni milioni 19 kumsaini mshambuliaji wa Uholanzi Donyell Malen, 25, kutoka Borussia Dortmund. (Athletic)

Villa pia wameanzisha mazungumzo na Sevilla huku wakitafuta kumsajili beki wa Ufaransa Loic Bade mwenye umri wa miaka 24. (L'Equipe)

Leicester wanajiandaa kumsajili mlinzi wa pembeni wa Ufaransa Woyo Coulibaly, 25, kutoka Parma kwa mkataba wa pauni milioni 3. (Fabrizio Romano)

Chelsea itamruhusu kiungo Carney Chukwuemeka, 21, kuondoka kwa mkopo mwezi huu, huku Borussia Dortmund na Strasbourg zikimuwania. (Fabrizio Romano)

Nottingham Forest iko tayari kupokea ofa kwa ajili mshambuliaji Emmanuel Dennis, 27, klabu zenye nia zinazoshiriki Ligi ya Mabingwa, Serie A na La Liga. (Sky Sports)

Beki wa Ureno Renato Veiga, 21, ana uwezekano wa kuondoka Chelsea mwezi Januari, huku klabu za Uingereza, Ujerumani, Ufaransa na Italia zikionesha nia ya kumpata. (Athletic)

Monaco wametoa pendekezo la pili kwa West Ham kwa ajili ya Edson Alvarez, 27, baada ya ofa yao ya awali ya mkopo kwa kiungo huyo wa Mexico kugonga mwamba. (Mail)

Beki wa Uholanzi Tyrell Malacia, 25, anaweza kuondoka Manchester United kwa mkataba wa mkopo mwezi huu. (Fabrizio Romano)

Real Madrid wanaangalia uwezekano wa kuchagua wasimamizi kuchukua nafasi ya Carlo Ancelotti baada ya kufungwa 5-2 na Barcelona kwenye fainali ya Spanish Super Cup. (Relevo)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
47m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’