Klabu ya Simba imethibitisha adhabu kutoka kwa Shirikisho la Mpira wa miguu barani Afrika (CAF) ambapo imezuiwa kuingiza mashabiki katika mchezo ujao wa kombe la Shirikisho dhidi ya CS Constantine ambao utapigwa Jumapili, Januari 19 uwanja wa Benjamin Mkapa
Adhabu hii ni kutokana na vurugu zilizojitokeza katika mchezo uliopita nyumbani dhidi ya CS Sfaxine
Simba pia imetozwa faini ya dola 40,000 (zaidi ya Tsh 100M)



